President Samia Suluhu Hassan with Tundu Lissu in Belgium

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Samia Suluhu Hassan amekutana leo na kufanya mazungumzo mafupi na Makamu Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Mhe. Tundu Lissu.

Mhe. Rais Samia Suluhu Hassan akiwa na Makamu Mwenyekiti Wa Chadema, Mhe. Tundu Lissu jijini Brussels nchini Ubelgiji.

Mazungumzo hayo yamefanyika baada ya Rais Samia ambaye pia ni Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) kukubali maombi ya kiongozi huyo wa Chadema kukutana naye na kuzungumza jijini Brussels nchini Ubelgiji.

Aidha katika mazungumzo hayo Mhe. Rais na Makamu Mwenyekiti wa Chadema, Tundu Lissu, walizungumza masuala mbalimbali yenye maslahi na ustawi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Ni ishara ya upendo kati ya Mhe. Rais Samia na Mhe. Tundu Lissu walipokutana jijini Brussels.

Mhe. Tundu Lissu, alikuwa mgombea wa Urais katika uchaguzi mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania mwaka 2015 kupitia Chadema.

Previous articleMwenyekiti Wa Simba Afurahishwa Na Uwezo Wa Timu Yake
Next articleFreeman Mbowe Na Wenzake Wakutwa Na Kesi Ya Kujibu