Rais Magufuli

Leo ni maadhimisho ya mwaka mmoja tangu Rais wa awamu ya tano wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt John Pombe Joseph Magufuli afariki dunia. Maadhimisho hayo yanafanyika mkoani Geita katika wilaya ya Chato.

Wanajeshi wa jeshi la ulinzi Tanzania wakibeba jeneza lililobeba mwili wa hayati Magufuli.

Maadhimisho hayo yatahudhuriwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mh. Samia Suluhu Hassan, Makamu wa Rais, Dkt. Isdori Mpango, Waziri Mkuu, Mh. Majaliwa Kassim Majaliwa.

Viongozi mbalimbali wa serikali wakiwa na maafisa usalama wakati wa mazishi ya Rais Magufuli.

Viongozi wengine watakaoshiriki katika maadhimisho hayo ni Spika wa Bunge la Tanzania, Dkt. Tulia Ackson, Jaji Mkuu, Profesa Ibrahim Juma, Rais wa Zanzibar, Dkt. Hussein Mwinyi na viongozi wengine mbalimbali wa serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Mjane wa Rais Magufuli akilia kwa uchungu siku ya kumuaga hayati Magufuli.
Previous articleTanzania Yandoa Sharti La Kuwa Na Cheti Cha PCR Kwa Wasafiri
Next articleDiamond Platnumz – Gidi