Democratic Presidential candidate Joe Biden speaks at the Chase Center in Wilmington, Delaware, on November 4, 2020. - President Donald Trump and Democratic challenger Joe Biden are squaring off for what could be a legal battle for the White House, running neck-and-neck in the electoral vote count, and several battleground states still in play on November 4. (Photo by JIM WATSON / AFP) (Photo by JIM WATSON/AFP via Getty Images)

Makamu wa rais wa zamani, Joseph Robinette Biden Jr., amechaguliwa kuwa rais wa 46 wa Marekani. Ushindi wa rais mteule Joe Biden, umetangazwa na vyombo mbalimbali vya habari nchini Marekani baada ya kufikisha kura 270 ambazo zinatakiwa kufikishwa kwa mgombea yeyote ili ashinde urais wa nchi hiyo.

Kutokana na ushindi huu, inamfanya kuwa rais mwenye umri mkubwa zaidi kuchaguliwa kuongoza taifa hilo tajiri la kiuchumi na kijeshi duniani.

Kamala Harris ambaye ni mgombea mwenza wa Joe Biden, anakuwa makamu wa rais wa kwanza mwanamke kwa Marekani na pia makamu wa rais wa kwanza ambaye sio mzungu bali ni mchanganyiko wa muhindi na mjamaica.

Ushindi wa Joe Biden kutoka chama cha Democratic, unahitimisha urais wa Donald J. Trump wa chama cha Republican ambaye anakuwa rais tano kwa nchi hiyo kupoteza uchaguzi baada ya kugombea kwa ajili ya kutaka kuongoza muhula wa pili wa urais.

Ramani inayoonyesha matokeo ya Urais Marekani yanavyoonyesha jinsi Joe Biden na Rais Donald Trump walivyoshinda katika majimbo mbalimbali.

Baada ya kutangazwa matokeo hayo, wamarekani kutoka miji mbalimbali wameingia mitaani kuanza kushangilia kuondolewa madarakani kwa rais Donald Trump.

People celebrate Saturday, Nov. 7, 2020, in Philadelphia, after Democrat Joe Biden defeated President Donald Trump to become 46th president of the United States. (AP Photo/Rebecca Blackwell)
Previous articleDr. Dre Divorce: Estranged Wife Wants To Know If He Had Kids Outside Marriage
Next articleSocialite And Zimbabwean Businessman Ginimbi Kadungure Dies in Car Accident